
LOML | Love Of My Life (55)


ππππ (π³πππ ππ ππ ππππ) β£οΈ:55
Sio kitu kibaya lakini nafikiri mtu ukipendwa vizuri hata usiposema watu wao wenyewe watajua tu kuwa una amani na furaha kwa maisha yako.
Hii mume wangu amefanya hivi, mume wangu hawezi nisaliti, mume wangu ameleta hiki, kikapanda kikashuka ni kama kutangaza vita na shetani.
Kwasababu hujui mtu unamwambia, una muelezea ni nani, anawaza nini kwaajili yako. Watu wengine maneno yao tu ndani ya moyo ni mabaya juu yako.
Kama ilivyo pesa inakaa kwenye heshima na ndoa hivyohivyo inalindwa kwa heshima. Ni vizuri sana kuheshimu kila kitu na sio kumkaribisha shetani.
Nilitoka zangu bafuni, mke wangu alikuwa na furaha na kusema vile anaongea na rafiki yake akimtaja jina lake βGiana huyo!!β
Nilitabasamu na kusema βanasemaje shemeji yangu.β
Alinitazama na kusema βatasema nini tena, leo anatoka na mume wake basi ananitambia.β
Nilitabasamu nikisema βwewe sasa unatakiwa kutulia mpaka ujifungue nitakupeleka Paris.β
Mke wangu alinitazama na kusema βmmh unanitania si ndiyo?β
Nilicheka na kusema βkwanini nikutanie, nataka kukufanya mwanamke mwenye furaha hapa duniani. Nataka nikupende sana Gabriella. Wewe ni mke wangu.β
Mke wangu kwa madeko alisema βwako, peke yako, waoooo nasubiri kwa hamu. Nijifungue tu jamani.β
Nilicheka nikisema βmpaka mwisho wa mwaka huko, tulia tu.β
Alisikitika kidogo na kudeka akisema βhata hivyo sio mbali, nitafika lazima. I love you Dadie.β
Nilitabasamu na kusema βI love you mamie.β
Alinikumbatia na kunibusu. Unajua tena watoto wa wenye pesa madeko madeko tena hapa ndiyo kwake. Gabriella wangu anadeka sana.
BaΕΔ± siku hii ilikuwa siku nzuri sana, siku yenge furaha, maana tulifanya kila kitu ambacho ndoa yenye furaha inatakiwa kuwa nacho. Nyumba ilitabasamu, ilishangilia nyumba ilikuwa nzuri sana nakumbuka.