LOML | Love Of My Life (64)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:64
Jamani natetemeka, mke wangu sijui ni changudoa au ni nani. Mke wangu ni mshenzi, Malaya mbwa akasome. Nilisema kabla sijakutwa na hii Hali natetemeka nachukua hii namba ya mtu huyu nitamtafuta. Nikaanza ingiza kwa simu yangu.

Ile namna na mimi ninayo, ni Max, huyu ni msimamizi wa ndoa yetu, ni kama kama kwangu. Anafanya kazi kwa kampuni yangu miaka na miaka Kumbe anakula mke wangu, Kumbe analala na mke wangu, na kuhusu mimba ndiyo sielewi nachanganyikiwa.

Mtu pekee ambaye nikishindwa kote ushauri wa ndoa yangu una muhitaji kumbe ndiyo kwanza ana muingilia mke wangu kotekote tu hajali hata kuhusu hili. Dunia aina huruma.

Nilijikaza niendelee kuangalia, nashindwa niseme nini, hata dokta ambaye mimi nilimpeleka alishalala naye tena kotekote tu mke wangu nikitembea naona nachekwa, halafu wananicheka kuwa mimi Kumbe sio hata Mlaji nikajibebesha msumari ni mshamba.

Dokta ambaye alikuwa ananiambia madhara na mbaya Kwa Mungu, kwa sheria leo hii yeye mwenyewe na mke wangu ni walewale. Naishiwa nguvu hata kulia siwezi.

Başı nataka kurudisha simu maana moyo unapasuka, unavuja damu niliona namba haina jina, nikafungua hapo nilichokiona nilichoka, Mc wa ndoa yetu mke wangu ameshalala naye, amelala naye na picha zipo hapa wametumiana wakiambiana ni namna gani wamekumbukana.

Nilijihamishia kila kitu, kisha nikafuta nilichoona ambacho yeye hakuona. Halafu niliondoka zangu chumbani nimechanganyikiwa. Ile natoka naona mke wangu huyu hapa. Nilizidi kuchukia, aliniita β€œmume wangu!!, upo sawa?”
Nilishusha pumzi na kusema β€œNarudi sasa hivi.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata