LOML | Love Of My Life (69)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:69
Pina aliniachia ingawaje mimi nilikuwa natamani hili kumbato liendelee Tena na Tena na tena, nilimshika mkono, yeye uso wake ulikuwa usoni kwangu tu na aliniambia β€œPole sana Rodricky, nimewahi kuwa kwa hali kama yako, nimewahi kujisikia hivyohivyo. Lakini sasa nipo hapa. Ninatabasamu na ninayo amani.”

Nilimtazama, mara nilisikia Mlio wa simu ndogo hizi nokia torch. Alijipapasa kiunoni, na kisha alipokea na kusema β€œhello.”

Upande wa pili alizungumza nini mimi sijui lakini yeye alisema β€œUsijali kabisa bibi, nipo salama. Nitarudi sio muda. Nimekutana na rafiki ananihitaji. Nikizungumza naye nitarudi hapo haraka. Naomba nisamehe sana bibi yangu mrembo kuliko mabibi wote duniani.”

Nilijikuta natabasamu vile anaongea ana furaha sana na tabasamu La kutosha. Na vile amesema amekutana na rafiki anahitaji kumsikiliza. Halafu alipomaliza alikuwa anatabasamu bado akisema β€œbibi yangu, tunaweza kutoka hapa sasa Rodricky?”

Nilimshika mkono, na hakubisha taratibu tulianza kutoka na nilimuongoza mpaka kwa gari. Nilimfungulia mlango wa gari, nikamsaidia kuingia na kisha na Mimi nikazunguka upande wa pili na kuingia.

Nilimsaidia msichana huyu mzuri kumfunga mkanda na kisha aliniambia β€œnimekuamini.”
Nilitabasamu na kusema β€œnakuahidi sitakufanya jambo lolote baya.”
Aliniambia tena β€œMazingira ni haya haya hakuna kuondoka hapa tafadhali.”
Nilimtazama na kusema β€œhakuna shida, Hakuna shida kabisa.”

Nilisogeza tu gari ili Ikae sehemu nzuri maana Mungu peke yake ndiyo anajua namna nimefika hapa na kisha nilisimamisha gari. Nikawa tu namtazama huyu mrembo usoni. Alinyamaza kimya tu.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

BIKIRA YA BIBI HARUSI FULL

BINTI MDUNGUAJI FULL

KIAPO CHA MASIKINI FULL

KIBOKO YANGU FULL