
LOML | Love Of My Life (73)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:73
Nililia sana, nililia kwa muda na hata nikawa tu napumua kwa nguvu. Na Pina msichana mstaarabu huyu aliniambia โtafadhali tulia, tulia tafadhali Ricky, nakuomba.โ
Nilimshika mikono yake milaini na kwa upendo nikaikumbatia na kusema โnashukuru sana Pina. Sikujua kama nitakuona tena leo, sikujua kama tutaonana.โ
Pina alinitazama na kusema โulisema umewahi kuniona kabla.โ
Nilimtazama kwa upole nikasema โndiyo hapahapa kanisani, lakini sikukuona tena?โ
Akaniuliza akinishangaa โina maana ulikuwa unanitafuta?, kwanini?โ
Nilishindwa kujibu badala yake nikisema โsijui ila nilikuwa natamani kuzungumza na wewe, siamini leo kama nimezungumza na wewe Pina.โ
Alishusha pumzi na kusema โRicky, unakumbuka ndani nilisema nini?โ
Nilimtazama tu na kisha nilimjibu โnikumbushe tafadhali.โ
Alivuta pumzi na kisha kwa upole alisema โmtu ni mtu tu, siku zote atakuwa hivyo huchukua muda sana mtu huyu kuwa binadamu.โ
Nilimtazama na kisha aliendelea โkuna watu wanafanya mambo kwasababu tu wameamua kufanya, ndiyo aina ya maisha wamejichagulia. Wanajisikia kupata amani na kufurahia wakifanya hivyo.
Ni hulka zao kamwe huwezi badili au kuzuia ndiyo alivyo. Na wengine ni maumivu yamebadilisha tabia zao na kuona kila kitu ni sawa tu mwenye maisha yao. Lakini kubwa na zaidi watu wengi sana hawana Mungu ndani yao.
Kumkosa Mungu, hata ile hofu ya Mungu kwenye maisha ni mzigo mkubwa sana. Utafanya mambo ya kutisha na utaona kawaida kabisa na wala hutomuelewa mtu yeyote yule akikushauri kuwa unachofanya ni kitu kibaya.
Sitaki nikusumbue na maneno mengi sana Ricky kwa siku ya Leo. Unatakiwa kunyamaza, unatakiwa kujikaza wewe ni mwanaume na ile ni nyumba yako. Rodricky pale ni nyumbani kwako na huwezi kubadilisha kuwa yule ni mke wako lazima mtakaa pamoja, lazima mtazungumza.

