
SEASON 3: LOML | Love Of My Life (117)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:117
Nilisoma, nilisoma kwa kumuhurumia lakini Sikutaka kumzingatia, Mara uliingia mwingine โnipo nyumbani mume wangu, usinitelekeze kama hunijui. Naomba tuzungumze mume wangu. Nakuomba uje kunichukua.โ
Nilisoma tu na kuona nachanganyikiwa. Niliamua kumpigia simu rafiki yangu Willy. Willy alipokea simu yangu na kusema โkaka Upo wapi?โ
Nilimwambia kwa upole โUpo wapi?, leo nataka kunywa kidogo.โ
Willy alicheka mna Kisha aliniuliza โkwema?โ
Nilimwambia kwa kusema โhata sielewi kabisa, nataka tuonane tu nipunguze mawazo.โ
Willy aliniambia โnakufuata hapo sio muda. Jiandae.โ
Nilivuta pumzi na kusema โfanya haraka.โ
Akaniambia kwa upole โnaacha garฤฑ nakuja na pikipiki.โ
Nilimtazama na kusema โni sawa, Hakuna shida.โ
Nilitoka nje mpaka kwa gari yangu, nilikaa nimejiinamia tu. Kiukweli sina raha kabisa, maisha yangu yote naona Hakuna raha naipata. Nilisubiri kwa muda, na Kisha rafiki yangu alifika.
Nilimfungulia mlango wa gari na akaingia, aliponiona tu, nilijikuta machozi yananitoka sana. Alinikumbatia kwa nguvu, akinipigapiga mgongoni na mimi nikiongea kwa uchungu โnajikaza kaka nashindwa nashindwa kabisa.โ
Willy alinituliza sana, Kisha aliondoa gari. Alinipeleka mpaka ufukweni. Nakumbuka sana. Tulishuka na hata nikamuuliza โumenileta hapa kufanya nini kaka?, nataka kulewa.โ
Alinitazama na kuniambia โwewe ni ndugu yangu, siwezi kukupeleka kulewa kama sehemu ya kรผpรผnguza maumivu yako. Kaa hapa, Ila unavyotaka ukimaliza nakuomba niambie nini kinasumbua.โ
Nilimtazama na kusema kwa upole โmke wangu kaka, mke wangu.โ
Willy alishangaa na kuniuliza โmke wako?, mbona mlikuwa na furaha sana leo pale ndani.โ

