SEASON 3: LOML | Love Of My Life (117)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:117
Nilisoma, nilisoma kwa kumuhurumia lakini Sikutaka kumzingatia, Mara uliingia mwingine β€œnipo nyumbani mume wangu, usinitelekeze kama hunijui. Naomba tuzungumze mume wangu. Nakuomba uje kunichukua.”

Nilisoma tu na kuona nachanganyikiwa. Niliamua kumpigia simu rafiki yangu Willy. Willy alipokea simu yangu na kusema β€œkaka Upo wapi?”
Nilimwambia kwa upole β€œUpo wapi?, leo nataka kunywa kidogo.”

Willy alicheka mna Kisha aliniuliza β€œkwema?”
Nilimwambia kwa kusema β€œhata sielewi kabisa, nataka tuonane tu nipunguze mawazo.”
Willy aliniambia β€œnakufuata hapo sio muda. Jiandae.”

Nilivuta pumzi na kusema β€œfanya haraka.”
Akaniambia kwa upole β€œnaacha garΔ± nakuja na pikipiki.”
Nilimtazama na kusema β€œni sawa, Hakuna shida.”

Nilitoka nje mpaka kwa gari yangu, nilikaa nimejiinamia tu. Kiukweli sina raha kabisa, maisha yangu yote naona Hakuna raha naipata. Nilisubiri kwa muda, na Kisha rafiki yangu alifika.

Nilimfungulia mlango wa gari na akaingia, aliponiona tu, nilijikuta machozi yananitoka sana. Alinikumbatia kwa nguvu, akinipigapiga mgongoni na mimi nikiongea kwa uchungu β€œnajikaza kaka nashindwa nashindwa kabisa.”

Willy alinituliza sana, Kisha aliondoa gari. Alinipeleka mpaka ufukweni. Nakumbuka sana. Tulishuka na hata nikamuuliza β€œumenileta hapa kufanya nini kaka?, nataka kulewa.”

Alinitazama na kuniambia β€œwewe ni ndugu yangu, siwezi kukupeleka kulewa kama sehemu ya kΓΌpΓΌnguza maumivu yako. Kaa hapa, Ila unavyotaka ukimaliza nakuomba niambie nini kinasumbua.”

Nilimtazama na kusema kwa upole β€œmke wangu kaka, mke wangu.”
Willy alishangaa na kuniuliza β€œmke wako?, mbona mlikuwa na furaha sana leo pale ndani.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

BINTI MDUNGUAJI FULL

LOML | Love Of My Life FULL

JOGGING MASTER FULL

CHAGUO LA MOYO FULL