
SEASON 5: LOML | Love Of My Life (207)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:207
Baba alitabasamu tu. Nilimshika mkono mpaka chumbani kwangu. Nilipofika huko nilimshika vizuri na kumuuliza “Upo sawa mpenzi ?”
Aliniambia kwa upole “Nipo sawa mpenzi. Ninakuacha uwe huru na baba wakati mimi namalizia uzingizi wangu Kisha mkimaliza nirudi nyumbani kesho nitakuja kukuona tena si ni sawa?”
Nilimtazama na kusema “nilijua utalala eti?”
Alitabasamu na kusema “sio leo mpenzi ungekuwa unaumwa bado sawa.”
Nilicheka nikisema “huoni naumwa sana ujue Pina wangu.”
Tulijikuta tunacheka tu.Kisha mimi nilitoka na kumuacha Pina kitandani.
Baba yangu aliponiona natabasamu na yeye alitabasamu na kusema “anaonekana ni binti mzuri sana. Ana heshima na upendo sana. Sijui kwanini Ila Nina furaha sana nikikuona na huyu binti. Mtafika mbali sana.”
Nilitabasamu na kusema “baba Nina furaha sana. Hata sijui kwanini nilikuwa nachelewa kuwa naye. Yeye ni kila kitu nahitaji kwenye maisha yangu.”
Baba alicheka kidogo na kusema “ndiyo ukamuoa tena kikokoteo.”
Nilicheka na kusema “baba una nini lakini?”
Baba alisema “sasa tuseme nini na wakati sijui yeye ndiyo mwanaume au mwanamke. Yule binti ni mchawi nashukuru Mungu hajakuua mwanangu.”
Nilishusha pumzi, baba alisema “nilikuja kukuona na nafurahi kuona unaendelea vizuri. Lakini pia namba ya mwanasheria mzuri wa mambo ya taraka huyu hapa mwanangu.
Atakusidia kıla kiti nishazungumza naye unajua cha kufanya. zaidi ya hapo ni kanisani na ukweli sasa ndiyo utakuweka huru. Muhimu unajiondoa kwa kifungo hiki. Nadhani unanielewa kijana wangu.”
Nilimkumbatia baba na kusema “baba wewe ndiyo kila kitu. Nafurahia sana unavyo niunga mkono. Natumaini siku moja mama atanielewa na tutakuwa na furaha sana.”

