
SEASON 5: LOML | Love Of My Life (207)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:207
Baba alitabasamu tu. Nilimshika mkono mpaka chumbani kwangu. Nilipofika huko nilimshika vizuri na kumuuliza โUpo sawa mpenzi ?โ
Aliniambia kwa upole โNipo sawa mpenzi. Ninakuacha uwe huru na baba wakati mimi namalizia uzingizi wangu Kisha mkimaliza nirudi nyumbani kesho nitakuja kukuona tena si ni sawa?โ
Nilimtazama na kusema โnilijua utalala eti?โ
Alitabasamu na kusema โsio leo mpenzi ungekuwa unaumwa bado sawa.โ
Nilicheka nikisema โhuoni naumwa sana ujue Pina wangu.โ
Tulijikuta tunacheka tu.Kisha mimi nilitoka na kumuacha Pina kitandani.
Baba yangu aliponiona natabasamu na yeye alitabasamu na kusema โanaonekana ni binti mzuri sana. Ana heshima na upendo sana. Sijui kwanini Ila Nina furaha sana nikikuona na huyu binti. Mtafika mbali sana.โ
Nilitabasamu na kusema โbaba Nina furaha sana. Hata sijui kwanini nilikuwa nachelewa kuwa naye. Yeye ni kila kitu nahitaji kwenye maisha yangu.โ
Baba alicheka kidogo na kusema โndiyo ukamuoa tena kikokoteo.โ
Nilicheka na kusema โbaba una nini lakini?โ
Baba alisema โsasa tuseme nini na wakati sijui yeye ndiyo mwanaume au mwanamke. Yule binti ni mchawi nashukuru Mungu hajakuua mwanangu.โ
Nilishusha pumzi, baba alisema โnilikuja kukuona na nafurahi kuona unaendelea vizuri. Lakini pia namba ya mwanasheria mzuri wa mambo ya taraka huyu hapa mwanangu.
Atakusidia kฤฑla kiti nishazungumza naye unajua cha kufanya. zaidi ya hapo ni kanisani na ukweli sasa ndiyo utakuweka huru. Muhimu unajiondoa kwa kifungo hiki. Nadhani unanielewa kijana wangu.โ
Nilimkumbatia baba na kusema โbaba wewe ndiyo kila kitu. Nafurahia sana unavyo niunga mkono. Natumaini siku moja mama atanielewa na tutakuwa na furaha sana.โ

